Simba Fisi na Sungura
Simba Fisi na Sungura

Harakati za Simba, Fisi, na Sungura

Orodha ya Yaliyomo

Hapo zamani za kale simba aliyejulikana kama Sim’ba, fisi aliyejulikana kama Fee’see na sungura aliyejulikana kama Keetee’tee waliamua kufanya shughuli ya kilimo. Hivyo waliamua kwenda kijijini, wakatengeneza bustani, na kupanda kila aina ya pembejeo, kisha walirudi nyumbani na kupumzika.

Wakati ulipowadia ambapo mazao yao yalikuwa tayari kwa kuvunwa, walianza kuambiana, “Hebu twendeni shambani tukaone hali ya mazao yetu.”

Makubaliano

Hivyo basi, asubuhi moja, mapema sana walianza safari, na kwakuwa bustani yao ilikuwa mbali, sungura aliyejulikana kwa jina la Keetee’tee, alitoa ombi lake: “Wakati tukielekea shambani, tusisimame njiani; na kama mmoja wetu akisimama, basi na ageuzwe kitoweo.” Kwakuwa wenzake hawakuwa wajanja kama yeye, na kwakuwa walifikiri ya kwamba wataweza kumshinda, walikubaliana na matakwa yake.

Hivyo, waliendelea na safari; lakini hawakuwa wamefika mbali mara sungura akasimama.

“Hullo!” alisema fisi ambaye alijulikana kwa jina la Fee’see, “Katee’tee kasimama. Inabidi aliwe.”

“Hayo ndiyo makubaliano,” simba aliyejulikana kwa jina la Sim’ba aliitikia.

“Mnajua,” alisema sungura, “Nilikuwa nikiwaza.”

“Kuhusu nini?” waliuliza wenzake, wakiwa na shauku kubwa.

Ujanga wa Sungura

“Ninawaza,” allijibu sungura, kwa mafumbo, “kuhusu hayo mawe mawili, moja ni kubwa na jingine ni dogo; hilo dogo halielekei juu, na wala hilo kubwa halielekea chini.”

Simba na fisi, wakiwa wamesimama kutazama hayo mawe, walisema, “Kwanini, kweli, ni umoja, lakini ni sawa kabisa na ulivyosema.” kisha wote wakaendelea na safari, wakati huo sungura alikuwa amekwisha kupumzika sana.

Simba, Fisi na Sungura walihamuwa kuanza kilimo
Simba, Fisi na Sungura walihamuwa kuanza kilimo

Wakiwa wametembea umbali kidogo, mara sungura akasimama tena.

“Aha!” akasema Fee’see, “Keetee’tee kasimama tena. Sasa lazima aliwe.”

“Hata mimi ninawaza hivyo,” simba aliitikia.

“Sawa,” alisema sungura, “Nilikuwa nikiwaza tena.”

Shauku yao ilikuwa juu sana, na wakaanza kumuomba awaeleze ni kitu gani anawaza.

“Kwanini,” Alisema sungura, “Nilikuwa nikiwaza kuhusu hili: Watu kama sisi tukivaa makoti mapya, je yale ya zamani huenda wapi?”

Sim’ba na fee’see wakiwa nao wamesimama huku wakitafakari hilo suala, wakapiga kelele kwa pamoja, “Ndiyo, nashangaa pia!” and wote watatu wakaendelea na safari, huku sungura kwa mara nyingine akiwa ameweza kupumzika.

Jaribio la Fisi kumgeza Sungura

Baada ya muda mfupi, fisi akiwa naye amehisi ni muda sahihi wa kuonyesha uwezo wake wa kifalsafa, alisimama ghafla.

“Sasa,” alifoka Sim’ba, “haitasaidia; ninadhani hatunabudi kukula Fee’see.”

“Oh, hapana,” alisema fisi; “Nilikuwa nikiwaza.”

“Unawaza kitu gani?” waliuliza kwa pamoja.

Alisema Fisi, Ninafikiria
Alisema Fisi, Ninafikiria

“Sina ninachowaza kabisa,” alijibu fisi, akiwa anajitanabahi kuwa mjanja sana na mwenye akili.

“Ah, pshaw!” Keetee’tee alitoa mlio,”hatudanganyiki kwa njia hiyo.”

Kuliwa kwa Simba na Fisi

Hivyo basi yeye na Sim’ba walimla fisi.

Walipomaliza kumla rafiki yao, simba na sungura waliendelea na safari, na wakawa wamefika kwenye eneo ambapo kulikuwa na pango, na hapo sungura akasimama.

“H’m!” akaguna Sim’ba; “Sina njaa kama niliyokuwa nayo asubuhi, ila nadhani ninaweza kupata nafasi kwa ajili yako, dogo dogo Keetee’tee.”

“Oh, nina Imani haiwezekani,” alijibu Ketee’tee, “Ninawaza tena.”

“Ndiyo,” alisema sim’ba, “kitu gani sasa?”

Sungura alijibu: “ Ninafikiri kuhusu pango. Hapo zamani mababu zetu walikuwa wanaingilia hapa, na wanatokea kule, na sasa ninafikiri nitajaribu na kufuata njia zao.”

Hivyo sungura aliingia kwenye pango kwa kupitia upande mmoja na kutokea upande mwingine kwa kurudia zoezi hili mara kadhaa.

Kisha akamwamboa simba, “Sim’ba, rafiki yangu wa siku nyingi, hebu tuone nawe ukijaribu kufanya kama nilivyofanya,” simba akaingia kwenye pango, lakini mara akanaswa na kushindwa kwenda mbele wala kurudi nyuma.

Bila kupoteza muda Keetee’tee alimrukia Sim’ba mgongoni na kisha kuuanza kumla.

Baada ya muda kidogo simba akapiga kelele, “Jamani, kaka yangu, hebu jaribu kufanya usawa; njoo pia ule sehemu yangu ya mbele.”

sungura
sungura

Lakini sungura akamjibu, “Ukweli ni kwamba siwezi kuja huko mbele, kwakuwa ninaona haya kukutazama usoni.”

Baada ya kula kiasi alichoweza, aliondoka akimuacha simba pale, na kwenda kuwa mmiliki pekee wa shamba na mazao yote.

Kwa nakala zaidi zinazohusu hadithi bofya hapa!